Swahili New Testament Bible

Matthew 6

Matthew

Return to Index

Chapter 7

1


 

  "Msiwahukumu wengine, msije nanyi mkahukumiwa na Mungu;  

 

 

--

2


 

  kwa maana jinsi mnavyowahukumu wengine, ndivyo nanyi mtakavyohukumiwa; na kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho Mungu atakachotumia kwenu.  

 

 

--

3


 

  Kwa nini wakiona kibanzi kilicho jichoni mwa ndugu yako, na papo hapo huioni boriti iliyoko jichoni mwako?  

 

 

--

4


 

  Au, wawezaje kumwambia ndugu yako, `Ndugu, ngoja nikuondoe kibanzi jichoni mwako`, wakati wewe mwenyewe unayo boriti jichoni mwako?  

 

 

--

5


 

  Mnafiki wewe! Ondoa kwanza boriti iliyoko jichoni mwako na hapo ndipo utaona waziwazi kiasi cha kuweza kuondoa kibanzi kilichoko jichoni mwa ndugu yako.  

 

 

--

6


 

  "Msiwape mbwa vitu vitakatifu wasije wakageuka na kuwararua ninyi; wala msiwatupie nguruwe lulu zenu wasije wakazikanyaga.  

 

 

--

7


 

  "Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtapata; bisheni, nanyi mtafunguliwa.  

 

 

--

8


 

  Maana, aombaye hupewa, atafutaye hupata, na abishaye hufunguliwa.  

 

 

--

9


 

  Je, kuna yeyote miongoni mwenu ambaye mtoto wake akimwomba mkate, atampa jiwe?  

 

 

--

10


 

  Au je, akimwomba samaki, atampa nyoka?  

 

 

--

11


 

  Kama basi ninyi, ingawa ni waovu, mwajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, hakika Baba yenu wa mbinguni atafanya zaidi: atawapa mema wale wanaomwomba.  

 

 

--

12


 

  "Watendeeni wengine yale mnayotaka wao wawatendee ninyi. Hii ndiyo maana ya Sheria ya Mose na mafundisho ya manabii.  

 

 

--

13


 

  "Ingieni kwa kupitia mlango mwembamba. Kwa maana njia inayoongoza kwenye maangamizi ni pana, na mlango wa kuingilia humo ni mpana; waendao njia hiyo ni wengi.  

 

 

--

14


 

  Lakini njia inayoongoza kwenye uzima ni nyembamba, na mlango wa kuingilia humo ni mwembamba; ni watu wachache tu wanaoweza kuigundua njia hiyo.  

 

 

--

15


 

  "Jihadharini na manabii wa uongo. Wao huja kwenu wakionekana kama kondoo kwa nje, lakini kwa ndani ni mbwa mwitu wakali.  

 

 

--

16


 

  Mtawatambua kwa matendo yao. Je, watu huchuma zabibu katika miti ya miiba, au tini katika mbigili? La!  

 

 

--

17


 

  Basi, mti mwema huzaa matunda mema, na mti mbaya huzaa matunda mabaya.  

 

 

--

18


 

  Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mbaya hauwezi kuzaa matunda mema.  

 

 

--

19


 

  Kila mti usiozaa matunda mema utakatwa na kutupwa motoni.  

 

 

--

20


 

  Kwa hiyo, mtawatambua kwa matendo yao. ic  

 

 

--

21


 

  "Si kila aniambiaye, `Bwana, Bwana,` ataingia katika Ufalme wa mbinguni; ila ni yule tu anayetimiza mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.  

 

 

--

22


 

  Wengi wataniambia Siku ile ya hukumu: `Bwana, Bwana! kwa jina lako tulitangaza ujumbe wako, na kwa jina lako tuliwatoa pepo na kufanya miujiza mingi.`  

 

 

--

23


 

  Hapo nitawaambia: `Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni mbele yangu, enyi watenda maovu.`  

 

 

--

24


 

  "Kwa sababu hiyo, kila mtu anayeyasikia maneno yangu na kuyazingatia, anafanana na mtu mwenye busara, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba.  

 

 

--

25


 

  Mvua ikanyesha, mito ikafurika, pepo kali zikavuma na kuipiga nyumba hiyo. Lakini haikuanguka kwa sababu ilikuwa imejengwa juu ya mwamba.  

 

 

--

26


 

  "Lakini yeyote anayesikia maneno yangu haya bila kuyazingatia, anafanana na mtu mpumbavu aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga.  

 

 

--

27


 

  Mvua ikanyesha, mito ikafurika, pepo kali zikavuma na kuipiga nyumba hiyo, nayo ikaanguka; tena kwa kishindo kikubwa."  

 

 

--

28


 

  Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, umati wa watu ukashangazwa na mafundisho yake.  

 

 

--

29


 

  Hakuwa kama walimu wao wa Sheria, bali alifundisha kwa mamlaka.  

 

 

--

Matthew 8

 

 

 

 

HTMLBible Software - Public Domain Software by johnhurt.com

 


Other Items are Available At These Sites: