Swahili New Testament Bible

Matthew 9

Matthew

Return to Index

Chapter 10

1


 

  Yesu aliwaita wanafunzi wake kumi na wawili, akawapa uwezo wa kutoa pepo wachafu na kuponya magonjwa na maradhi yote.  

 

 

--

2


 

  Majina ya hao mitume kumi na wawili ni haya: wa kwanza ni Simoni aitwae Petro, na Andrea ndugu yake; Yakobo mwana wa Zebedayo, na Yohane ndugu yake;  

 

 

--

3


 

  Filipo na Bartholomayo, Thoma na Mathayo aliyekuwa mtoza ushuru; Yakobo mwana wa Alfayo, na Thadayo;  

 

 

--

4


 

  Simoni Mkanaani, na Yuda Iskarioti ambaye alimsaliti Yesu.  

 

 

--

5


 

  Yesu aliwatuma hao kumi na wawili na kuwapa maagizo haya: "Msiende kwa watu wa mataifa mengine, wala msiingie katika mji wa Wasamaria.  

 

 

--

6


 

  Ila nendeni kwa watu wa Israeli waliopotea kama kondoo.  

 

 

--

7


 

  Mnapokwenda hubirini hivi: `Ufalme wa mbinguni umekaribia.`  

 

 

--

8


 

  Ponyeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo. Mmepewa bure, toeni bure.  

 

 

--

9


 

  Msichukue mifukoni mwenu dhahabu, wala fedha, wala sarafu za shaba.  

 

 

--

10


 

  Msichukue mkoba wa kuombea njiani, wala koti la ziada, wala viatu, wala fimbo. Maana mfanyakazi anastahili riziki yake.  

 

 

--

11


 

  "Mkiingia katika mji wowote au kijiji, tafuteni humo mtu yeyote aliye tayari kuwakaribisheni, na kaeni naye mpaka mtakapoondoka mahali hapo.  

 

 

--

12


 

  Mnapoingia nyumbani wasalimuni wenyeji wake.  

 

 

--

13


 

  Kama wenyeji wa nyumba hiyo wakiipokea salamu hiyo, basi, amani yenu itakaa pamoja nao. Lakini ikiwa hawaipokei, basi amani yenu itawarudia ninyi.  

 

 

--

14


 

  Kama mtu yeyote atakataa kuwakaribisheni au kuwasikilizeni, basi mtokapo katika nyumba hiyo au mji huo, yakung`uteni mavumbi miguuni mwenu kama onyo kwao.  

 

 

--

15


 

  Kweli nawaambieni, Siku ya hukumu mji huo utapata adhabu kubwa kuliko ile iliyoipata miji ya Sodoma na Gomora.  

 

 

--

16


 

  "Sasa, mimi nawatuma ninyi kama kondoo kati ya mbwa mwitu. Muwe na busara kama nyoka, na wapole kama njiwa.  

 

 

--

17


 

  Jihadharini na watu, maana watawapeleka ninyi mahakamani na kuwapiga viboko katika masunagogi yao.  

 

 

--

18


 

  Mtapelekwa mbele ya watawala na wafalme kwa sababu yangu, mpate kutangaza Habari Njema kwao na kwa mataifa.  

 

 

--

19


 

  Basi, watakapowapeleka ninyi mahakamani, msiwe na wasiwasi mtasema nini au namna gani; wakati utakapofika, mtapewa la kusema.  

 

 

--

20


 

  Maana si ninyi mtakaosema, bali ni Roho wa Baba yenu asemaye ndani yenu.  

 

 

--

21


 

  "Ndugu atamsaliti ndugu yake auawe, na baba atamsaliti mwanawe, nao watoto watawashambulia wazazi wao na kuwaua.  

 

 

--

22


 

  Watu wote watawachukieni kwa sababu ya jina langu. Lakini atakayevumilia mpaka mwisho, ataokolewa.  

 

 

--

23


 

  "Watu wakiwadhulumu katika mji mmoja, kimbilieni mji mwingine. Kweli nawaambieni, hamtamaliza ziara yenu katika miji yote ya Israeli kabla Mwana wa Mtu hajafika.  

 

 

--

24


 

  "Mwanafunzi si mkuu kuliko mwalimu wake, wala mtumishi si mkuu kuliko bwana wake.  

 

 

--

25


 

  Yatosha mwanafunzi kuwa kama mwalimu wake, na mtumishi kuwa kama bwana wake. Ikiwa wamemwita mkubwa wa jamaa Beelzebuli, je hawatawaita watu wengine wa jamaa hiyo majina mabaya zaidi?  

 

 

--

26


 

  "Basi, msiwaogope watu hao. Kila kilichofunikwa kitafunuliwa, na kila kilichofichwa kitafichuliwa.  

 

 

--

27


 

  Ninalowaambieni ninyi katika giza, lisemeni katika mwanga; na jambo mlilosikia likinong`onezwa, litangazeni hadharani.  

 

 

--

28


 

  Msiwaogope wale wauao mwili, lakini hawawezi kuiua roho. Afadhali zaidi kumwogopa yule awezaye kuuangamiza mwili pamoja na roho katika moto wa Jehanamu.  

 

 

--

29


 

  Shomoro wawili huuzwa kwa senti tano. Lakini hata mmoja wao haanguki chini bila kibali cha Baba yenu.  

 

 

--

30


 

  Lakini kwa upande wenu, hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote.  

 

 

--

31


 

  Kwa hiyo msiogope; ninyi mu wa thamani kuliko shomoro wengi. ic  

 

 

--

32


 

  "Kila mtu anayekiri hadharani kwamba yeye ni wangu, mimi pia nitamkiri mbele ya Baba yangu aliye mbinguni.  

 

 

--

33


 

  Lakini yeyote atakayenikana hadharani, nami nitamkana mbele ya Baba yangu aliye mbinguni.  

 

 

--

34


 

  "Msidhani kwamba nimekuja kuleta amani duniani. Sikuja kuleta amani bali upanga.  

 

 

--

35


 

  Maana nimekuja kuleta mafarakano kati ya mtu na baba yake, kati ya binti na mama yake, kati ya mkwe na mkwe wake.  

 

 

--

36


 

  Na maadui wa mtu ni watu wa nyumbani mwake.  

 

 

--

37


 

  "Ampendaye baba au mama yake kuliko anipendavyo mimi, hanistahili. Ampendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili.  

 

 

--

38


 

  Mtu asiyechukua msalaba wake na kunifuata, hanistahili.  

 

 

--

39


 

  Anayeyashikilia maisha yake, atayapoteza; lakini anayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu, atayapata.  

 

 

--

40


 

  "Anayewakaribisha ninyi, ananikaribisha mimi; na anayenikaribisha mimi, anamkaribisha yule aliyenituma.  

 

 

--

41


 

  Anayemkaribisha nabii kwa sababu ni nabii, atapokea tuzo la nabii. Anayemkaribisha mtu mwema kwa sababu ni mtu mwema, atapokea tuzo la mtu mwema.  

 

 

--

42


 

  Kweli nawaambieni, yeyote atakayempa mmojawapo wa wadogo hawa kikombe cha maji baridi kwa sababu ni mfuasi wangu, hatakosa kamwe kupata tuzo lake."  

 

 

--

Matthew 11

 

 

 

 

HTMLBible Software - Public Domain Software by johnhurt.com

 


Other Items are Available At These Sites: