Swahili New Testament Bible

Matthew 13

Matthew

Return to Index

Chapter 14

1


 

  Wakati huo, mtawala Herode alisikia sifa za Yesu.  

 

 

--

2


 

  Basi, akawaambia watumishi wake, "Mtu huyu ni Yohane mbatizaji, amefufuka kutoka wafu; ndiyo maana nguvu za miujiza zinafanya kazi ndani yake."  

 

 

--

3


 

  Herode ndiye aliyekuwa amemtia Yohane nguvuni, akamfunga minyororo na kumtia gerezani kwa sababu ya Herodia, mke wa Filipo, ndugu yake. Sababu hasa ni  

 

 

--

4


 

  kwamba alikuwa amemwambia Herode, "Si halali kwako kuishi na huyo mwanamke!"  

 

 

--

5


 

  Herode alitaka kumwua Yohane, lakini aliogopa watu kwa sababu kwao Yohane alikuwa nabii.  

 

 

--

6


 

  Katika sherehe za sikukuu ya kuzaliwa kwake Herode, binti ya Herodia alicheza mbele ya wageni. Herode alifurahiwa,  

 

 

--

7


 

  hata akaahidi kwa kiapo kumpa huyo msichana chochote atakachoomba.  

 

 

--

8


 

  Naye, huku akichochewa na mama yake, akaomba, "Nipe papahapa katika sinia kichwa cha Yohane mbatizaji."  

 

 

--

9


 

  Mfalme alihuzunika, lakini kwa sababu ya kile kiapo chake na kwa sababu ya wale wageni karamuni, akaamuru apewe.  

 

 

--

10


 

  Basi, Herode akatuma mtu gerezani amkate kichwa Yohane.  

 

 

--

11


 

  Kichwa chake kikaletwa katika sinia, wakampa yule msichana, naye akampelekea mama yake.  

 

 

--

12


 

  Wanafunzi wa Yohane wakaja, wakauchukua mwili wake, wakauzika. Kisha wakaenda kumpasha habari Yesu.  

 

 

--

13


 

  Yesu alipopata habari hiyo, aliondoka mahali pale kwa mashua, akaenda mahali pa faragha peke yake. Lakini watu walipata habari, wakamfuata kwa miguu toka mijini.  

 

 

--

14


 

  Basi, aliposhuka pwani, aliona umati mkubwa wa watu, akawaonea huruma, akawaponya wagonjwa wao.  

 

 

--

15


 

  Kulipokuwa jioni, wanafunzi wake walimwendea wakamwambia, "Mahali hapa ni nyikani, na saa zimepita. Basi, uwaage watu ili waende vijijini wakajinunulie chakula."  

 

 

--

16


 

  Yesu akawaambia, "Si lazima waende, wapeni ninyi chakula."  

 

 

--

17


 

  Lakini wao wakamwambia, "Tunayo mikate mitano tu na samaki wawili."  

 

 

--

18


 

  Yesu akawaambia, "Nileteeni hapa."  

 

 

--

19


 

  Akawaamuru watu waketi katika nyasi. Kisha akaitwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akamshukuru Mungu. Halafu akaimega hiyo mikate, akawapa wanafunzi wake, nao wakawapa watu.  

 

 

--

20


 

  Watu wote wakala, wakashiba. Kisha wanafunzi wakakusanya mabaki, wakajaza vikapu kumi na viwili.  

 

 

--

21


 

  Jumla ya waliokula ilikuwa wanaume wapatao elfu tano, bila kuhesabu wanawake na watoto.  

 

 

--

22


 

  Mara, Yesu akawaamuru wanafunzi wake wapande mashua, wamtangulie ng`ambo ya ziwa wakati yeye anawaaga watu.  

 

 

--

23


 

  Baada ya kuwaaga, alipanda mlimani peke yake kusali. Ilipokuwa jioni, yeye alikuwa huko peke yake,  

 

 

--

24


 

  na wakati huo ile mashua ilikwishafika karibu katikati ya ziwa, lakini ilikuwa inakwenda mrama kwa sababu upepo ulikuwa unaipinga.  

 

 

--

25


 

  Usiku, karibu na mapambazuko, Yesu aliwaendea wanafunzi akitembea juu ya maji.  

 

 

--

26


 

  Wanafunzi wake walipomwona akitembea juu ya maji waliingiwa na hofu, wakasema, "Ni mzimu!" Wakapiga kelele kwa hofu.  

 

 

--

27


 

  Mara, Yesu akasema nao, "Tulieni, ni mimi. Msiogope!"  

 

 

--

28


 

  Petro akamwambia, "Bwana, ikiwa ni wewe kweli, amuru nitembee juu ya maji nije kwako."  

 

 

--

29


 

  Yesu akasema, "Haya, njoo." Basi, Petro akashuka kutoka ile mashua, akatembea juu ya maji, akamwendea Yesu.  

 

 

--

30


 

  Lakini alipouona ule upepo, aliogopa, akaanza kuzama; akalia kwa sauti, "Bwana, niokoe!"  

 

 

--

31


 

  Hapo, Yesu akaunyosha mkono wake, akamshika na kumwambia, "Ewe mwenye imani haba! Kwa nini uliona shaka?"  

 

 

--

32


 

  Basi, wakapanda mashuani, na upepo ukatulia.  

 

 

--

33


 

  Wote waliokuwa ndani ya mashua walimsujudia, wakasema, "Hakika wewe ni Mwana wa Mungu."  

 

 

--

34


 

  Walivuka ziwa, wakafika nchi ya Genesareti.  

 

 

--

35


 

  Watu wa huko walipomtambua, wakaeneza habari pote katika sehemu hizo. Basi, wakamletea Yesu wagonjwa wote,  

 

 

--

36


 

  wakamwomba awaruhusu waguse tu pindo la vazi lake; wote waliomgusa walipona.  

 

 

--

Matthew 15

 

 

 

 

HTMLBible Software - Public Domain Software by johnhurt.com

 


Other Items are Available At These Sites: