Swahili New Testament Bible

Matthew 24

Matthew

Return to Index

Chapter 25

1


 

  "Wakati huo, Ufalme wa mbinguni utafanana na wasichana kumi waliochukua taa zao, wakaenda kumlaki bwana arusi.  

 

 

--

2


 

  Watano miongoni mwao walikuwa wapumbavu na watano walikuwa wenye busara.  

 

 

--

3


 

  Wale wapumbavu walichukua taa zao, lakini hawakuchukua akiba ya mafuta.  

 

 

--

4


 

  Lakini wale wenye busara walichukua mafuta katika chupa pamoja na taa zao.  

 

 

--

5


 

  Kwa kuwa bwana arusi alikawia kuja, wale wanawali wote wote walisinzia, wakalala.  

 

 

--

6


 

  Usiku wa manane kukawa na kelele: `Haya, haya! Bwana arusi anakuja; nendeni kumlaki.`  

 

 

--

7


 

  Hapo wale wanawali wote wakaamka, wakazitayarisha taa zao.  

 

 

--

8


 

  Wale wapumbavu wakawaambia wale wenye busara: `Tupeni mafuta yenu kidogo maana taa zetu zinazimika.`  

 

 

--

9


 

  Lakini wale wenye busara wakawaambia, `Hayatatutosha sisi na ninyi! Afadhali mwende dukani mkajinunulie wenyewe!`  

 

 

--

10


 

  Basi, wale wanawali wapumbavu walipokwenda kununua mafuta, bwana arusi akafika, na wale wanawali waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye katika jumba la arusi, kisha mlango ukafungwa.  

 

 

--

11


 

  Baadaye wale wanawali wengine wakaja, wakaita: `Bwana, bwana, tufungulie!`  

 

 

--

12


 

  Lakini yeye akawajibu, `Nawaambieni kweli, siwajui ninyi."`  

 

 

--

13


 

  Kisha Yesu akasema, "Kesheni basi, kwa maana hamjui siku wala saa.  

 

 

--

14


 

  "Itakuwa kama mtu mmoja aliyetaka kusafiri ng`ambo: aliwaita watumishi wake, akawakabidhi mali yake.  

 

 

--

15


 

  Alimpa kila mmoja kadiri ya uwezo wake: mmoja sarafu tano za fedha ziitwazo talanta, mwingine talanta mbili na mwingine talanta moja, kisha akasafiri.  

 

 

--

16


 

  Mara yule aliyekabidhiwa talanta tano akafanya kazi nazo akapata faida talanta tano.  

 

 

--

17


 

  Hali kadhalika na yule aliyekabidhiwa talanta mbili akapata faida talanta mbili.  

 

 

--

18


 

  Lakini yule aliyekabidhiwa talanta moja akaenda akachimba shimo ardhini, akaificha fedha ya bwana wake.  

 

 

--

19


 

  "Baada ya muda mrefu, yule bwana alirudi, akaanza kukagua hesabu ya matumizi na mapato ya fedha yake.  

 

 

--

20


 

  Mtumishi aliyekabidhiwa talanta tano akaja amechukua zile talanta tano faida, akamwambia, `Bwana, ulinikabidhi talanta tano, hapa pana talanta tano zaidi faida niliyopata.`  

 

 

--

21


 

  Bwana wake akamwambia, `Vema, mtumishi mwema na mwaminifu. Umekuwa mwaminifu katika mambo madogo nitakukabidhi makubwa. Njoo ufurahi pamoja na bwana wako.`  

 

 

--

22


 

  "Mtumishi aliyekabidhiwa talanta mbili akaja, akatoa talanta mbili faida, akisema, `Bwana, ulinikabidhi talanta mbili. Chukua talanta mbili zaidi faida niliyopata.`  

 

 

--

23


 

  Bwana wake akamwambia, `Vema, mtumishi mwema na mwaminifu. Umekuwa mwaminifu katika mambo madogo, nitakukabidhi makubwa. Njoo ufurahi pamoja na bwana wako.`  

 

 

--

24


 

  "Lakini yule aliyekabidhiwa talanta moja akaja, akasema, `Bwana, najua wewe ni mtu mgumu; wewe huvuna pale ambapo hukupanda, na kukusanya pale ambapo hukutawanya.  

 

 

--

25


 

  Niliogopa, nikaificha fedha yako katika ardhi. Chukua basi mali yako.`  

 

 

--

26


 

  "Bwana wake akamwambia, `Wewe ni mtumishi mwovu na mvivu! Unajua kuwa mimi huvuna mahali ambapo sikupanda, na hukusanya pale ambapo sikutawanya.  

 

 

--

27


 

  Ilikupasa basi, kuiweka fedha yangu katika benki, nami ningelichukua mtaji wangu na faida yake!  

 

 

--

28


 

  Basi, mnyang`anyeni hiyo fedha mkampe yule mwenye talanta kumi.  

 

 

--

29


 

  Maana, aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.  

 

 

--

30


 

  Na kuhusu huyu mtumishi asiye na faida, mtupeni nje gizani! Huko kutakuwa na kilio na kusaga meno.`  

 

 

--

31


 

  "Wakati Mwana wa Mtu atakapokuja katika utukufu wake na malaika wote wakiwa pamoja naye, hapo ataketi juu ya kiti chake cha enzi kitukufu,  

 

 

--

32


 

  na mataifa yote yatakusanyika mbele yake, naye atawatenganisha watu kama mchungaji anavyotenganisha kondoo na mbuzi.  

 

 

--

33


 

  Atawaweka kondoo upande wake wa kulia na mbuzi upande wake wa kushoto.  

 

 

--

34


 

  "Kisha Mfalme atawaambia wale walio upande wake wa kulia, `Njoni enyi mliobarikiwa na Baba yangu; pokeeni Ufalme mliotayarishiwa tangu kuumbwa kwa ulimwengu.  

 

 

--

35


 

  Maana nilikuwa na njaa nanyi mkanipa chakula; nilikuwa na kiu nanyi mkanipa maji; nilikuwa mgeni nanyi mkanikaribisha;  

 

 

--

36


 

  nilikuwa uchi, mkanivika; nilikuwa mgonjwa nanyi mkaja kunitazama; nilikuwa gerezani nanyi mkaja kunitembelea.`  

 

 

--

37


 

  Hapo, hao watu wema watamjibu mfalme `Bwana, ni lini tulikuona mwenye njaa nasi tukakupa chakula, au ukiwa na kiu nasi tukakunywesha maji?  

 

 

--

38


 

  Ni lini tulikuona ukiwa mgeni nasi tukakukaribisha, au bila nguo nasi tukakuvika?  

 

 

--

39


 

  Ni lini tulikuona ukiwa mgonjwa au mfungwa nasi tukaja kukutazama?`  

 

 

--

40


 

  Mfalme atawajibu, `Kweli nawaambieni, kila kitu mlichomtendea mmojawapo wa hawa ndugu zangu wadogo, mlinitendea mimi.`  

 

 

--

41


 

  "Kisha atawaambia wale walio upande wake wa kushoto, `Ondokeni mbele yangu enyi mliolaaniwa! Nendeni katika moto wa milele aliotayarishiwa Ibilisi na malaika wake.  

 

 

--

42


 

  Maana nilikuwa na njaa nanyi hamkunipa chakula; nilikuwa na kiu nanyi hamkunipa maji.  

 

 

--

43


 

  Nilikuwa mgeni nanyi hamkunikaribisha; nilikuwa mgonjwa na mfungwa nanyi hamkuja kunitazama.`  

 

 

--

44


 

  "Hapo nao watajibu, `Bwana, ni lini tulikuona ukiwa na njaa au kiu, ukiwa mgeni au bila nguo, ukiwa mgonjwa au mfungwa, nasi hatukuja kukuhudumia?`  

 

 

--

45


 

  Naye atawajibu, `Nawaambieni kweli, kila mlipokataa kumtendea mambo haya mmojawapo wa hawa wadogo, mlikataa kunitendea mimi.`  

 

 

--

46


 

  Basi, hawa watakwenda kwenye adhabu ya milele, lakini wale waadilifu watakwenda kwenye uzima wa milele."  

 

 

--

Matthew 26

 

 

 

 

HTMLBible Software - Public Domain Software by johnhurt.com

 


Other Items are Available At These Sites: