Swahili New Testament Bible

Mark 12

Mark

Return to Index

Chapter 13

1


 

  Yesu alipokuwa anatoka Hekaluni, mmoja wa wanafunzi wake alimwambia, "Mwalimu, tazama jinsi mawe haya na majengo haya yalivyo ya ajabu!"  

 

 

--

2


 

  Yesu akamwambia, "Je, unayaona majengo haya makubwa? Hakuna hata jiwe moja litakalosalia juu ya lingine; kila kitu kitabomolewa."  

 

 

--

3


 

  Yesu alipokuwa ameketi juu ya mlima wa Mizeituni akielekea Hekalu, Petro, Yakobo, Yohane na Andrea wakamwuliza kwa faragha,  

 

 

--

4


 

  "Twambie mambo haya yatatukia lini? Ni ishara gani itakayoonyesha kwamba mambo haya karibu yatimizwe?"  

 

 

--

5


 

  Yesu akaanza kuwaambia, "Jihadharini msije mkadanganywa na mtu.  

 

 

--

6


 

  Maana wengi watakuja wakilitumia jina langu, wakisema, `Mimi ndiye!` nao watawapotosha watu wengi.  

 

 

--

7


 

  Mtakaposikia juu ya vita na fununu za vita, msifadhaike. Mambo hayo lazima yatokee, lakini mwisho wenyewe ungali bado.  

 

 

--

8


 

  Taifa moja litapigana na taifa lingine; utawala mmoja utapigana na utawala mwingine; kila mahali kutakuwa na mitetemeko ya ardhi na njaa. Mambo haya ni kama tu maumivu ya kwanza ya kujifungua mtoto.  

 

 

--

9


 

  "Lakini ninyi jihadharini. Maana watu watawapelekeni mahakamani, na kuwapigeni katika masunagogi. Mtapelekwa mbele ya watawala na wafalme kwa sababu yangu ili mpate kunishuhudia kwao.  

 

 

--

10


 

  Lakini lazima kwanza Habari Njema ihubiriwe kwa mataifa yote.  

 

 

--

11


 

  Nao watakapowatieni nguvuni na kuwapeleka mahakamani, msiwe na wasiwasi juu ya yale mtakayosema; saa ile itakapofika, semeni chochote mtakachopewa, maana si ninyi mtakaosema, bali Roho Mtakatifu.  

 

 

--

12


 

  Ndugu atamsaliti ndugu yake auawe; baba atamsaliti mwanae; watoto watawashambulia wazazi wao na kuwaua.  

 

 

--

13


 

  Watu wote watawachukieni ninyi kwa sababu ya jina langu. Lakini atakayevumilia mpaka mwisho ndiye atakayeokolewa.  

 

 

--

14


 

  "Mtakapoona `Chukizo Haribifu` limesimama mahali ambapo si pake, (msomaji na atambue maana yake!) Hapo watu walioko Yudea wakimbilie milimani.  

 

 

--

15


 

  Mtu aliye juu ya paa la nyumba asishuke kuingia nyumbani mwake kuchukua kitu.  

 

 

--

16


 

  Aliye shambani asirudi nyuma kuchukua vazi lake.  

 

 

--

17


 

  Ole wao waja wazito na wanaonyonyesha siku hizo!  

 

 

--

18


 

  Ombeni ili mambo hayo yasitukie nyakati za baridi.  

 

 

--

19


 

  Maana wakati huo kutakuwa na dhiki ambayo haijatokea tangu Mungu alipoumba ulimwengu mpaka leo, wala haitatokea tena.  

 

 

--

20


 

  Kama Bwana asingepunguza siku hizo, hakuna binadamu ambaye angeokolewa. Lakini kwa ajili ya wateule wake, Bwana amezipunguza siku hizo.  

 

 

--

21


 

  "Basi mtu akiwaambieni, `Tazama, Kristo yupo hapa!` au `Yupo pale!` msimsadiki.  

 

 

--

22


 

  Maana watatokea kina Kristo wa uongo na manabii wa uongo, watafanya ishara na maajabu, ili kuwapotosha wateule wa Mungu, kama ikiwezekana.  

 

 

--

23


 

  Lakini ninyi jihadharini. Mimi nimewaambieni mambo yote kabla hayajatokea.  

 

 

--

24


 

  "Basi, siku hizo baada ya dhiki hiyo, jua litatiwa giza na mwezi hautaangaza.  

 

 

--

25


 

  Nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu za mbingu zitatikiswa.  

 

 

--

26


 

  Hapo watamwona Mwana wa Mtu akija katika mawingu kwa nguvu nyingi na utukufu.  

 

 

--

27


 

  Kisha atawatuma malaika wake; atawakusanya wateule wake kutoka pande zote nne za dunia, kutoka mwisho wa dunia mpaka mwisho wa mbingu.  

 

 

--

28


 

  "Kwa mtini jifunzeni mfano huu: Mara tu matawi yake yanapoanza kuwa laini na kuchanua majani, mnajua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.  

 

 

--

29


 

  Hali kadhalika nanyi mtakapoona mambo hayo yakitendeka, jueni kwamba Mwana wa Mtu yuko karibu sana.  

 

 

--

30


 

  Nawaambieni kweli, kizazi hiki hakitapita kabla ya mambo hayo yote kutukia.  

 

 

--

31


 

  Mbingu na dunia zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.  

 

 

--

32


 

  "Lakini hakuna mtu ajuaye siku au saa hiyo itakuja lini; wala malaika wa mbinguni, wala Mwana; Baba peke yake ndiye ajuaye.  

 

 

--

33


 

  Muwe waangalifu na kesheni, maana hamjui wakati huo utafika lini.  

 

 

--

34


 

  Itakuwa kama mtu anayeondoka nyumbani kwenda safari akiwaachia watumishi wake madaraka, kila mmoja na kazi yake; akamwambia mlinzi wa mlango awe macho.  

 

 

--

35


 

  Kesheni, basi, kwa maana hamjui mwenye nyumba atarudi lini; huenda ikawa jioni, usiku wa manane, alfajiri au asubuhi.  

 

 

--

36


 

  Kesheni ili akija ghafla asije akawakuta mmelala.  

 

 

--

37


 

  Ninayowaambieni ninyi, nawaambia wote: Kesheni!"  

 

 

--

Mark 14

 

 

 

 

HTMLBible Software - Public Domain Software by johnhurt.com

 


Other Items are Available At These Sites: