Swahili New Testament Bible

Mark 16

Luke

Return to Index

Chapter 1

1


 

  Mheshimiwa Theofilo: Watu wengi wamejitahidi kuandika juu ya mambo yale yaliyotendeka kati yetu.  

 

 

--

2


 

  Waliandika kama tulivyoelezwa na wale walioyaona kwa macho yao tangu mwanzo, na waliotangaza ujumbe huo.  

 

 

--

3


 

  Inafaa nami pia, Mheshimiwa, baada ya kuchunguza kwa makini mambo yote tangu mwanzo, nikuandikie kwa mpango,  

 

 

--

4


 

  ili nawe uweze kujionea mwenyewe ukweli wa mambo yale uliyofundishwa.  

 

 

--

5


 

  Wakati Herode alipokuwa mfalme wa Yudea, kulikuwa na kuhani mmoja jina lake Zakaria, wa kikundi cha Abia. Mke wake alikuwa anaitwa Elisabeti, naye alikuwa wa ukoo wa kuhani Aroni.  

 

 

--

6


 

  Wote wawili walikuwa wanyofu mbele ya Mungu, wakiishi kwa kufuata amri na maagizo yote ya Bwana bila lawama.  

 

 

--

7


 

  Lakini hawakuwa wamejaliwa watoto kwa vile Elisabeti alikuwa tasa, nao wote wawili walikuwa wazee sana.  

 

 

--

8


 

  Siku moja, ilipokuwa zamu yake ya kutoa huduma ya ukuhani mbele ya Mungu,  

 

 

--

9


 

  Zakariya alichaguliwa kwa kura, kama ilivyokuwa desturi, kuingia hekaluni ili afukize ubani.  

 

 

--

10


 

  Watu, umati mkubwa, walikuwa wamekusanyika nje wanasali wakati huo wa kufukiza ubani.  

 

 

--

11


 

  Malaika wa Bwana akamtokea humo ndani, akasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia ubani.  

 

 

--

12


 

  Zakariya alipomwona alifadhaika, hofu ikamwingia.  

 

 

--

13


 

  Lakini malaika akamwambia, "Zakariya, usiogope, kwa maana sala yako imesikilizwa, na Elisabeti mkeo atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yohane.  

 

 

--

14


 

  Utakuwa na furaha kubwa na watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.  

 

 

--

15


 

  Atakuwa mkuu mbele ya Bwana. Hatakunywa divai wala kileo, atajazwa Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.  

 

 

--

16


 

  Atawaelekeza wengi wa watu wa Israeli kwa Bwana Mungu wao.  

 

 

--

17


 

  Atamtangulia Bwana akiongozwa na nguvu na roho kama Eliya. Atawapatanisha kina baba na watoto wao; atawafanya wasiotii wawe na fikira za uadilifu, na hivyo amtayarishie Bwana watu wake."  

 

 

--

18


 

  Zakariya akamwambia huyo malaika, "Ni kitu gani kitakachonihakikishia jambo hilo? Mimi ni mzee, hali kadhalika na mke wangu."  

 

 

--

19


 

  Malaika akamjibu, "Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele ya Mungu, na nimetumwa niseme nawe, nikuletee hii habari njema.  

 

 

--

20


 

  Sikiliza, utakuwa bubu kwa sababu huyasadiki haya maneno yatakayotimia kwa wakati wake. Hutaweza kusema mpaka hayo niliyokuambia yatakapotimia."  

 

 

--

21


 

  Wakati huo, wale watu walikuwa wanamngoja Zakariya huku wakishangaa juu ya kukawia kwake Hekaluni.  

 

 

--

22


 

  Alipotoka nje, hakuweza kusema nao. Ikawa dhahiri kwao kwamba alikuwa ameona maono Hekaluni. Lakini akawa anawapa ishara kwa mikono, akabaki bubu.  

 

 

--

23


 

  Zamu yake ya kuhudumu ilipokwisha, alirudi nyumbani.  

 

 

--

24


 

  Baadaye Elisabeti mkewe akapata mimba. Akajificha nyumbani kwa muda wa miezi mitano, akisema:  

 

 

--

25


 

  "Hivi ndivyo alivyonitendea Bwana; ameniangalia na kuniondolea aibu niliyokuwa nayo mbele ya watu."  

 

 

--

26


 

  Mnamo mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu aende kwenye mji uitwao Nazareti huko Galilaya,  

 

 

--

27


 

  kwa msichana mmoja aitwaye Maria, mchumba wa mtu mmoja jina lake Yosefu, wa ukoo wa Daudi.  

 

 

--

28


 

  Malaika akamwendea, akamwambia, "Salamu Maria! Umejaliwa neema nyingi! Bwana yu pamoja nawe."  

 

 

--

29


 

  Maria aliposikia maneno hayo alifadhaika sana, akawaza: maneno haya yanamaanisha nini?  

 

 

--

30


 

  Malaika akamwambia, "Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema.  

 

 

--

31


 

  Utachukua mimba, utamzaa mtoto wa kiume na utampa jina Yesu.  

 

 

--

32


 

  Yeye atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Mungu Mkuu. Bwana Mungu atampa kiti cha mfalme Daudi, babu yake.  

 

 

--

33


 

  Kwa hivyo atautawala ukoo wa Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho."  

 

 

--

34


 

  Maria akamjibu, "Yatawezekanaje hayo, hali mimi ni bikira?"  

 

 

--

35


 

  Malaika akamjibu, "Roho Mtakatifu atakushukia, na uwezo wake Mungu Mkuu utakujia kama kivuli; kwa sababu hiyo, mtoto atakayezaliwa ataitwa Mtakatifu, Mwana wa Mungu.  

 

 

--

36


 

  Ujue pia kwamba hata Elisabeti, jamaa yako, naye amepata mimba ingawa ni mzee, na sasa ni mwezi wa sita kwake yeye ambaye watu walimfahamu kuwa tasa.  

 

 

--

37


 

  Kwa maana hakuna jambo lisilowezekana kwa Mungu."  

 

 

--

38


 

  Maria akasema, "Mimi ni mtumishi wa Bwana, nitendewe kama ulivyosema." Kisha yule malaika akaenda zake.  

 

 

--

39


 

  Siku kadhaa baadaye, Maria alifunga safari akaenda kwa haraka hadi mji mmoja ulioko katika milima ya Yuda.  

 

 

--

40


 

  Huko, aliingia katika nyumba ya Zakariya, akamsalimu Elisabeti.  

 

 

--

41


 

  Mara tu Elisabeti aliposikia sauti ya Maria, mtoto mchanga tumboni mwake Elisabeti akaruka. Naye Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifiu,  

 

 

--

42


 

  akasema kwa sauti kubwa, "Umebarikiwa kuliko wanawake wote, naye utakayemzaa amebarikiwa.  

 

 

--

43


 

  Mimi ni nani hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?  

 

 

--

44


 

  Nakwambia, mara tu niliposikia sauti yako, mtoto mchanga tumboni mwangu aliruka kwa furaha.  

 

 

--

45


 

  Heri yako wewe uliyesadiki kwamba yatatimia yale Bwana aliyokwambia."  

 

 

--

46


 

  Naye Maria akasema,  

 

 

--

47


 

  "Moyo wangu wamtukuza Bwana, roho yangu inafurahi kwa sababu ya Mungu Mwokozi wangu.  

 

 

--

48


 

  Kwa kuwa amemwangalia kwa huruma mtumishi wake mnyenyekevu. Hivyo tangu sasa watu wote wataniita mwenye heri.  

 

 

--

49


 

  Kwa kuwa Mwenyezi Mungu amenitendea makuu, jina lake ni takatifu.  

 

 

--

50


 

  Huruma yake kwa watu wanaomcha hudumu kizazi hata kizazi.  

 

 

--

51


 

  Amefanya mambo makuu kwa mkono wake: amewatawanya wenye kiburi katika mawazo ya mioyo yao;  

 

 

--

52


 

  amewashusha wenye nguvu kutoka vitu vyao vya enzi, akawakweza wanyenyekevu.  

 

 

--

53


 

  Wenye njaa amewashibisha mema, matajiri amewaacha waende mikono mitupu.  

 

 

--

54


 

  Amemsaidia Israeli mtumishi wake, akikumbuka huruma yake.  

 

 

--

55


 

  Kama alivyowaahidia wazee wetu Abrahamu na wazawa wake hata milele."  

 

 

--

56


 

  Maria alikaa na Elisabeti kwa muda upatao miezi mitatu, halafu akarudi nyumbani kwake.  

 

 

--

57


 

  Wakati wa kujifungua kwake Elisabeti ulifika, akajifungua mtoto wa kiume.  

 

 

--

58


 

  Jirani na watu wa jamaa yake walipopata habari kwamba Bwana amemwonea huruma kubwa, walifurahi pamoja naye.  

 

 

--

59


 

  Halafu siku ya nane walifika kumtahiri mtoto, wakataka kumpa jina la baba yake, Zakariya.  

 

 

--

60


 

  Lakini mama yake akasema, "La, sivyo, bali ataitwa Yohane."  

 

 

--

61


 

  Wakamwambia, "Mbona hakuna yeyote katika ukoo wake mwenye jina hilo?"  

 

 

--

62


 

  Basi, wakamwashiria baba yake wapate kujua alitaka mtoto wake apewe jina gani.  

 

 

--

63


 

  Naye akaomba kibao cha kuandikia, akaandika hivi: "Yohane ndilo jina lake." Wote wakastaajabu.  

 

 

--

64


 

  Papo hapo midomo na ulimi wake Zakariya vikafunguliwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.  

 

 

--

65


 

  Hofu ikawaingia jirani wote, na habari hizo zikaenea kila mahali katika milima ya Yudea.  

 

 

--

66


 

  Wote waliosikia mambo hayo waliyatafakari mioyoni mwao wakisema: "Mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?" Maana, hakika nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye.  

 

 

--

67


 

  Zakariya, baba yake mtoto, akajazwa Roho Mtakatifu, akatamka ujumbe wa Mungu:  

 

 

--

68


 

  "Asifiwe Bwana Mungu wa Israeli, kwani amekuja kuwasaidia na kuwakomboa watu wake.  

 

 

--

69


 

  Ametupatia Mwokozi shujaa, mzawa wa Daudi mtumishi wake.  

 

 

--

70


 

  Aliahidi hapo kale kwa njia ya manabii wake watakatifu,  

 

 

--

71


 

  kwamba atatuokoa mikononi mwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.  

 

 

--

72


 

  Alisema atawahurumia wazee wetu, na kukumbuka agano lake takatifu.  

 

 

--

73


 

  Kiapo alichomwapia Abrahamu baba yetu, ni kwamba atatujalia sisi  

 

 

--

74


 

  tukombolewe kutoka adui zetu, tupate kumtumikia bila hofu,  

 

 

--

75


 

  kwa unyofu na uadilifu mbele yake, siku zote za maisha yetu.  

 

 

--

76


 

  Nawe mwanangu, utaitwa, nabii wa Mungu Mkuu, utamtangulia Bwana kumtayarishia njia yake;  

 

 

--

77


 

  kuwatangazia watu kwamba wataokolewa kwa kuondolewa dhambi zao.  

 

 

--

78


 

  Mungu wetu ni mpole na mwenye huruma. Atasababisha pambazuko angavu la ukombozi litujie kutoka juu,  

 

 

--

79


 

  na kuwaangazia wote wanaokaa katika giza kuu la kifo, aongoze hatua zetu katika njia ya amani."  

 

 

--

80


 

  Mtoto akakua, akapata nguvu rohoni. Alikaa jangwani mpaka alipojionyesha rasmi kwa watu wa Israeli.  

 

 

--

Luke 2

 

 

 

 

HTMLBible Software - Public Domain Software by johnhurt.com

 


Other Items are Available At These Sites: