Swahili New Testament Bible

Luke 16

Luke

Return to Index

Chapter 17

1


 

  Kisha, Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Haiwezekani kabisa kusitokee vikwazo vinavyosababisha dhambi; lakini ole wake mtu yule atakayevisababisha.  

 

 

--

2


 

  Ingekuwa afadhali kwake kufungiwa shingoni jiwe kubwa la kusagia na kutoswa baharini, kuliko kumkwaza mmoja wa wadogo hawa.  

 

 

--

3


 

  Jihadharini! Kama ndugu yako akikukosea, mwonye; akitubu, msamehe.  

 

 

--

4


 

  Na kama akikukosea mara saba kwa siku, na kila mara akarudi kwako akisema `Nimetubu`, lazima umsamehe."  

 

 

--

5


 

  Mitume wakamwambia Bwana, "Utuongezee imani."  

 

 

--

6


 

  Naye Bwana akajibu, "Kama imani yenu ingekuwa ndogo hata kama chembe ndogo ya haradali, mngeweza kuuambia mti huu wa mkuyu: `Ng`oka ukajipandikize baharini`, nao ungewatii.  

 

 

--

7


 

  "Tuseme mmoja wenu ana mtumishi ambaye analima shambani au anachunga kondoo. Je, anaporudi kutoka shambani, atamwambia: `Haraka, njoo ule chakula?`  

 

 

--

8


 

  La! Atamwambia: `Nitayarishie chakula, ujifunge tayari kunitumikia mpaka nitakapomaliza kula na kunywa, ndipo nawe ule na unywe.`  

 

 

--

9


 

  Je utamshukuru huyo mtumishi kwa sababu ametimiza aliyoamriwa?  

 

 

--

10


 

  Hali kadhalika na ninyi mkisha fanya yote mliyoamriwa, semeni: `Sisi ni watumishi tusio na faida, tumetimiza tu yale tuliyotakiwa kufanya."`  

 

 

--

11


 

  Yesu akiwa safarini kwenda Yerusalemu alipitia mipakani mwa Samaria na Galilaya.  

 

 

--

12


 

  Alipokuwa anaingia katika kijiji kimoja, watu kumi wenye ukoma walikutana naye, wakasimama kwa mbali.  

 

 

--

13


 

  Wakapaza sauti wakisema, "Yesu Mwalimu, tuonee huruma!"  

 

 

--

14


 

  Alipowaona akawaambia, "Nendeni mkajionyeshe kwa makuhani." Basi, ikawa walipokuwa wanakwenda, wakatakasika.  

 

 

--

15


 

  Mmoja wao alipoona kwamba ameponywa alirudi akimtukuza Mungu kwa sauti kubwa.  

 

 

--

16


 

  Akajitupa chini mbele ya miguu ya Yesu huku akimshukuru. Huyo alikuwa Msamaria.  

 

 

--

17


 

  Hapo Yesu akasema, "Je, si watu kumi walitakaswa? Wale tisa wako wapi?  

 

 

--

18


 

  Hakupatikana mwingine aliyerudi kumtukuza Mungu ila tu huyu mgeni?"  

 

 

--

19


 

  Halafu akamwambia huyo mtu, "Simama, uende zako; imani yako imekuponya."  

 

 

--

20


 

  Wakati mmoja, Mafarisayo walimwuliza Yesu, "Ufalme wa Mungu utakuja lini?" Naye akawajibu, "Ufalme wa Mungu hauji kwa namna itakayoweza kuonekana.  

 

 

--

21


 

  Wala hakuna atakayeweza kusema, `Uko hapa`, au `Uko pale`. Kwa kweli Ufalme wa Mungu uko kati yenu."  

 

 

--

22


 

  Halafu akawaambia wanafunzi wake, "Siku zinakuja ambapo mtatamani kuona mojawapo ya siku za Mwana wa Mtu, lakini hamtaiona.  

 

 

--

23


 

  Na watu watawaambieni: `Tazameni yuko hapa`; ninyi msitoke wala msiwafuate.  

 

 

--

24


 

  Kwa maana kama vile umeme unavyotokea ghafla na kuangaza anga upande mmoja hadi mwingine, ndivyo Mwana wa Mtu atakavyokuwa siku yake.  

 

 

--

25


 

  Lakini kabla ya hayo, itambidi ateseke sana na kukataliwa na kizazi hiki.  

 

 

--

26


 

  Kama ilivyokuwa nyakati za Noa, ndivyo itakavyokuwa katika siku za Mwana wa Mtu.  

 

 

--

27


 

  Watu waliendelea kula na kunywa, kuoa na kuolewa mpaka wakati ule Noa alipoingia katika safina. Gharika ikatokea na kuwaangamiza wote.  

 

 

--

28


 

  Itakuwa kama ilivyotokea wakati wa Loti. Watu waliendelea kula na kunywa, kununua na kuuza, kupanda mbegu na kujenga.  

 

 

--

29


 

  Lakini siku ile Loti alipoondoka Sodoma, moto na kiberiti vikanyesha kama mvua kutoka mbinguni na kuwaangamiza wote.  

 

 

--

30


 

  Ndivyo itakavyokuwa siku ile Mwana wa Mtu atakapofunuliwa.  

 

 

--

31


 

  "Siku hiyo, yeyote atakayekuwa juu ya paa asishuke nyumbani kuchukua mali yake. Kadhalika, naye atakayekuwa shambani asirudi nyuma.  

 

 

--

32


 

  Kumbukeni yaliyompata mke wa Loti.  

 

 

--

33


 

  Yeyote anayetaka kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na yeyote anayeipoteza, ataiokoa.  

 

 

--

34


 

  Nawaambieni, siku ile usiku watu wawili watakuwa wanalala pamoja, mmoja atachukuliwa na yule mwingine ataachwa.  

 

 

--

35


 

  Wanawake wawili watakuwa wakisaga nafaka pamoja; mmoja atachukuliwa na mwingine ataachwa."*fc* atachukuliwa na mwingine ataachwa.\ie  

 

 

--

36


 

  missing  

 

 

--

37


 

  Hapo wakamwuliza, "Ni wapi Bwana?" Naye akawaambia, "Ulipo mzoga, ndipo tai watakapokusanyikia."  

 

 

--

Luke 18

 

 

 

 

HTMLBible Software - Public Domain Software by johnhurt.com

 


Other Items are Available At These Sites: