Swahili New Testament Bible

Luke 17

Luke

Return to Index

Chapter 18

1


 

  Basi, Yesu aliwasimulia mfano kuonyesha kwamba ni lazima kusali daima bila kukata tamaa.  

 

 

--

2


 

  Alisema: "Katika mji mmoja kulikuwa na hakimu ambaye hakuwa anamcha Mungu wala kumjali binadamu.  

 

 

--

3


 

  Katika mji huohuo, kulikuwa pia na mama mmoja mjane, ambaye alimwendea huyo hakimu mara nyingi akimwomba amtetee apate haki yake kutoka kwa adui yake.  

 

 

--

4


 

  Kwa muda mrefu huyo hakimu hakupenda kumtetea huyo mjane; lakini, mwishowe akajisemea: `Ingawa mimi simchi Mungu wala simjali binadamu,  

 

 

--

5


 

  lakini kwa vile huyu mjane ananisumbua, nitamtetea; la sivyo ataendelea kufika hapa, na mwisho atanichosha kabisa!"`  

 

 

--

6


 

  Basi, Bwana akaendelea kusema, "Sikieni jinsi alivyosema huyo hakimu mbaya.  

 

 

--

7


 

  Je, ndio kusema Mungu hatawatetea wale aliowachagua, ambao wanamlilia mchana na usiku? Je, atakawia kuwasikiliza?  

 

 

--

8


 

  Nawaambieni atawatetea upesi. Hata hivyo, je, kutakuwako na imani duniani wakati Mwana wa Mtu atakapokuja?"  

 

 

--

9


 

  Halafu Yesu aliwaambia pia mfano wa wale ambao walijiona kuwa wema na kuwadharau wengine.  

 

 

--

10


 

  "Watu wawili walipanda kwenda Hekaluni kusali: mmoja Mfarisayo, na mwingine mtoza ushuru.  

 

 

--

11


 

  Huyo Mfarisayo akasimama, akasali kimoyomoyo: `Ee Mungu, nakushukuru kwa vile mimi si kama watu wengine: walafi, wadanganyifu au wazinzi. Nakushukuru kwamba mimi si kama huyu mtoza ushuru.  

 

 

--

12


 

  Nafunga mara mbili kwa juma, natoa zaka sehemu ya kumi ya pato langu.`  

 

 

--

13


 

  Lakini yule mtoza ushuru, akiwa amesimama kwa mbali bila hata kuinua macho yake mbinguni, ila tu akijipiga kifua kwa huzuni, alisema: `Ee Mungu, unionee huruma mimi mwenye dhambi.`  

 

 

--

14


 

  Nawaambieni, huyu mtoza ushuru alirudi nyumbani akiwa amesamehewa. Lakini yule mwingine, sivyo. Kwa maana kila anayejikweza atashushwa, na kila anayejishusha atakwezwa."  

 

 

--

15


 

  Watu walimletea Yesu watoto wadogo ili awawekee mikono yake. Wanafunzi walipowaona, wakawazuia kwa maneno makali.  

 

 

--

16


 

  Lakini Yesu akawaita kwake akisema: "Waacheni hao watoto waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni kwa ajili ya watu kama hawa.  

 

 

--

17


 

  Nawaambieni kweli, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hataingia katika Ufalme huo."  

 

 

--

18


 

  Kiongozi mmoja, Myahudi, alimwuliza Yesu, "Mwalimu mwema, nifanye nini ili niweze kuupata uzima wa milele?"  

 

 

--

19


 

  Yesu akamwambia, "Mbona waniita mwema? Hakuna aliye mwema ila Mungu peke yake.  

 

 

--

20


 

  Unazijua amri: `Usizini; usiue; usiibe; usitoe ushahidi wa uongo; waheshimu baba yako na mama yako."`  

 

 

--

21


 

  Yeye akasema, "Hayo yote nimeyazingatia tangu ujana wangu."  

 

 

--

22


 

  Yesu aliposikia hayo akamwambia, "Unatakiwa bado kufanya kitu kimoja: uza kila ulicho nacho, wagawie maskini, na hivyo utakuwa na hazina yako mbinguni; halafu njoo unifuate."  

 

 

--

23


 

  Lakini huyo mtu aliposikia hayo, alihuzunika sana kwa sababu alikuwa tajiri sana.  

 

 

--

24


 

  Yesu alipoona akihuzunika hivyo, akasema, "Jinsi gani ilivyo vigumu kwa matajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu!  

 

 

--

25


 

  Naam, ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano, kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu."  

 

 

--

26


 

  Wale watu waliposikia hayo, wakasema, "Nani basi, atakayeokolewa?"  

 

 

--

27


 

  Yesu akajibu, "Yasiyowezekana kwa binadamu, yanawezekana kwa Mungu."  

 

 

--

28


 

  Naye Petro akamwuliza, "Na sisi je? Tumeacha vitu vyote tukakufuata!"  

 

 

--

29


 

  Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, mtu yeyote aliyeacha nyumba au mke au kaka au wazazi au watoto kwa ajili ya Ufalme wa Mungu,  

 

 

--

30


 

  atapokea mengi zaidi wakati huu wa sasa, na kupokea uzima wa milele wakati ujao."  

 

 

--

31


 

  Yesu aliwachukua kando wale kumi na wawili, akawaambia, "Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu na huko kila kitu kilichoandikwa na manabii kuhusu Mwana wa Mtu kitakamilishwa.  

 

 

--

32


 

  Kwa maana atakabidhiwa kwa watu wa mataifa nao watamtendea vibaya na kumtemea mate.  

 

 

--

33


 

  Watampiga mijeledi, watamuua; lakini siku ya tatu atafufuka."  

 

 

--

34


 

  Lakini wao hawakuelewa hata kidogo jambo hilo; walikuwa wamefichwa maana ya maneno hayo, na hawakutambua yaliyosemwa.  

 

 

--

35


 

  Wakati Yesu alipokaribia Yeriko, kulikuwa na mtu mmoja kipofu ameketi njiani akiomba.  

 

 

--

36


 

  Aliposikia umati wa watu ukipita aliuliza, "Kuna nini?"  

 

 

--

37


 

  Wakamwambia, "Yesu wa Nazareti anapita."  

 

 

--

38


 

  Naye akapaza sauti akisema, "Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!"  

 

 

--

39


 

  Wale watu waliotangulia wakamkemea wakimwambia anyamaze; lakini yeye akazidi kupaza sauti: "Mwana wa Daudi, nihurumie;"  

 

 

--

40


 

  Yesu alisimama, akaamuru wamlete mbele yake. Yule kipofu alipofika karibu, Yesu akamwuliza,  

 

 

--

41


 

  "Unataka nikufanyie nini?" Naye akamjibu, "Bwana, naomba nipate kuona tena."  

 

 

--

42


 

  Yesu akamwambia, "Ona! Imani yako imekuponya."  

 

 

--

43


 

  Na mara yule aliyekuwa kipofu akapata kuona, akamfuata Yesu akimtukuza Mungu. Watu wote walipoona hayo, wakamsifu Mungu.  

 

 

--

Luke 19

 

 

 

 

HTMLBible Software - Public Domain Software by johnhurt.com

 


Other Items are Available At These Sites: