Swahili New Testament Bible

Luke 24

John

Return to Index

Chapter 1

1


 

  Hapo Mwanzo, Neno alikuwako; naye alikuwa na Mungu, naye alikuwa Mungu.  

 

 

--

2


 

  Tangu mwanzo Neno alikuwa na Mungu.  

 

 

--

3


 

  Kwa njia yake vitu vyote viliumbwa; hakuna hata kiumbe kimoja kilichoumbwa pasipo yeye.  

 

 

--

4


 

  Yeye alikuwa chanzo cha uhai na uhai huo ulikuwa mwanga wa watu.  

 

 

--

5


 

  Na mwanga huo huangaza gizani, nalo giza halikuweza kuushinda.  

 

 

--

6


 

  Mungu alimtuma mtu mmoja jina lake Yohane,  

 

 

--

7


 

  ambaye alikuja kuwaambia watu juu ya huo mwanga. Alikuja ili kwa ujumbe wake watu wote wapate kuamini.  

 

 

--

8


 

  Yeye hakuwa huo mwanga, ila alikuja tu kuwaambia watu juu ya huo mwanga.  

 

 

--

9


 

  Huu ndio mwanga halisi, mwanga unaokuja ulimwenguni, na kuwaangazia watu wote.  

 

 

--

10


 

  Basi, Neno alikuwako ulimwenguni; na kwa njia yake ulimwengu uliumbwa, lakini ulimwengu haukumtambua.  

 

 

--

11


 

  Alikuja katika nchi yake mwenyewe, nao walio wake hawakumpokea.  

 

 

--

12


 

  Lakini wale wote waliompokea na kumwamini, hao aliwapa uwezo wa kuwa watoto wa Mungu.  

 

 

--

13


 

  Hawa wamekuwa watoto wa Mungu si kwa uwezo wa kibinadamu, wala kwa nguvu za kimwili, wala kwa mapenzi ya mtu, bali Mungu mwenyewe ndiye baba yao.  

 

 

--

14


 

  Naye Neno akawa mwanadamu, akakaa kwetu. Nasi tumeuona utukufu wake, utukufu wake yeye aliye Mwana wa pekee wa Baba; amejaa neema na ukweli.  

 

 

--

15


 

  Yohane aliwaambia watu habari zake, akasema kwa sauti, "Huyu ndiye niliyemtaja wakati niliposema: `Anakuja mtu mmoja baada yangu ambaye ni mkuu kuliko mimi, maana alikuwako kabla mimi sijazaliwa."`  

 

 

--

16


 

  Kutokana na ukamilifu wake sisi tumepokea neema mfululizo.  

 

 

--

17


 

  Maana Mungu alitoa Sheria kwa njia ya Mose, lakini neema na kweli vimekuja kwa njia ya Kristo.  

 

 

--

18


 

  Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wowote ule. Mwana wa pekee aliye sawa na Mungu ambaye ameungana na Baba, ndiye aliyetujulisha habari za Mungu.  

 

 

--

19


 

  Huu ndio ushahidi Yohane alioutoa wakati viongozi wa Wayahudi kule Yerusalemu walipowatuma makuhani wa Walawi kwake wamwulize: "Wewe u nani?"  

 

 

--

20


 

  Yohane hakukataa kujibu swali hilo, bali alisema waziwazi, "Mimi siye Kristo."  

 

 

--

21


 

  Hapo wakamwuliza, "Basi, wewe ni nani? Je, wewe ni Eliya?" Yohane akajibu, "La, mimi siye." Wakamwuliza, "Je, wewe ni yule nabii?" Yohane akawajibu, "La!"  

 

 

--

22


 

  Nao wakamwuliza, "Basi, wewe ni nani? Wasema nini juu yako mwenyewe? Tuambie, ili tuwapelekee jibu wale waliotutuma."  

 

 

--

23


 

  Yohane akawajibu, "Mimi ndiye yule ambaye nabii Isaya alisema habari zake: `Sauti ya mtu imesikika jangwani: Nyoosheni njia ya Bwana."`  

 

 

--

24


 

  Hao watu walikuwa wametumwa na Mafarisayo.  

 

 

--

25


 

  Basi, wakamwuliza Yohane, "Kama wewe si Kristo, wala Eliya, wala yule nabii, mbona wabatiza?"  

 

 

--

26


 

  Yohane akawajibu, "Mimi nabatiza kwa maji, lakini yuko mmoja kati yenu, msiyemjua bado.  

 

 

--

27


 

  Huyo anakuja baada yangu, lakini mimi sistahili hata kumfungua kamba za viatu vyake."  

 

 

--

28


 

  Mambo haya yalifanyika huko Bethania, ng`ambo ya mto Yordani ambako Yohane alikuwa anabatiza.  

 

 

--

29


 

  Kesho yake, Yohane alimwona Yesu akimjia, akasema, "Huyu ndiye Mwana-kondoo wa Mungu aondoaye dhambi ya ulimwengu!  

 

 

--

30


 

  Huyu ndiye niliyesema juu yake: `Baada yangu anakuja mtu mmoja aliye mkuu zaidi kuliko mimi, maana alikuwako kabla mimi sijazaliwa!`  

 

 

--

31


 

  Mimi mwenyewe sikumfahamu, lakini nimekuja kubatiza kwa maji ili watu wa Israeli wapate kumjua."  

 

 

--

32


 

  Huu ndio ushahidi Yohane alioutoa: "Nilimwona Roho akishuka kama njiwa kutoka mbinguni na kutua juu yake.  

 

 

--

33


 

  Mimi sikumjua, lakini yule aliyenituma nikabatize watu kwa maji alikuwa ameniambia: `Mtu yule utakayemwona Roho akimshukia kutoka mbinguni na kukaa juu yake, huyo ndiye anayebatiza kwa Roho Mtakatifu.`  

 

 

--

34


 

  Mimi nimeona na ninawaambieni kwamba huyu ndiye Mwana wa Mungu."  

 

 

--

35


 

  Kesho yake, Yohane alikuwa tena mahali hapo pamoja na wanafunzi wake wawili.  

 

 

--

36


 

  Alipomwona Yesu akipita akasema, "Tazameni! Huyu ndiye Mwana-kondoo wa Mungu."  

 

 

--

37


 

  Hao wanafunzi walimsikia Yohane akisema maneno hayo, wakamfuata Yesu.  

 

 

--

38


 

  Basi, Yesu aligeuka, na alipowaona hao wanafunzi wanamfuata, akawauliza, "Mnatafuta nini?" Nao wakamjibu, "Rabi (yaani Mwalimu), unakaa wapi?"  

 

 

--

39


 

  Yesu akawaambia, "Njoni, nanyi mtaona." Hao wanafunzi wakamfuata, wakaona mahali alipokuwa anakaa, wakashinda naye siku hiyo. Ilikuwa yapata saa kumi jioni.  

 

 

--

40


 

  Andrea, nduguye Simoni Petro, alikuwa mmoja wa hao wawili waliokuwa wamemsikia Yohane akisema hivyo, wakamfuata Yesu.  

 

 

--

41


 

  Andrea alimkuta kwanza Simoni, ndugu yake, akamwambia, "Tumemwona Masiha" (maana yake Kristo).  

 

 

--

42


 

  Kisha akampeleka Simoni kwa Yesu. Naye Yesu akamtazama Simoni akasema, "Wewe ni Simoni mwana wa Yohane. Sasa utaitwa Kefa." (maana yake ni Petro, yaani, "Mwamba.")  

 

 

--

43


 

  Kesho yake Yesu aliamua kwenda Galilaya. Basi, akamkuta Filipo, akamwambia, "Nifuate."  

 

 

--

44


 

  Filipo alikuwa mwenyeji wa Bethsaida, mji wa akina Andrea na Petro.  

 

 

--

45


 

  Naye Filipo akamkuta Nathanieli, akamwambia, "Tumemwona yule ambaye Mose aliandika juu yake katika kitabu cha Sheria, na ambaye manabii waliandika habari zake, yaani Yesu Mwana wa Yosefu, kutoka Nazareti."  

 

 

--

46


 

  Naye Nathanieli akamwuliza Filipo, "Je, kitu chema chaweza kutoka Nazareti?" Filipo akamwambia, "Njoo uone."  

 

 

--

47


 

  Yesu alipomwona Nathanieli akimjia alisema juu yake, "Tazameni! Huyo ni Mwisraeli halisi: hamna hila ndani yake."  

 

 

--

48


 

  Naye Nathanieli akamwuliza, "Umepataje kunijua?" Yesu akamwambia, "Ulipokuwa chini ya mtini hata kabla Filipo hajakuita, nilikuona."  

 

 

--

49


 

  Hapo Nathanieli akamwambia, "Mwalimu, wewe ni Mwana wa Mungu. Wewe ni Mfalme wa Israeli!"  

 

 

--

50


 

  Yesu akamwambia, "Je, umeamini kwa kuwa nimekwambia kwamba nilikuona chini ya mtini? Utaona makubwa zaidi kuliko haya."  

 

 

--

51


 

  Yesu akaendelea kusema, "Nawaambieni kweli, mtaona mbingu zinafunguka na malaika wa Mungu wakipanda na kushuka juu ya Mwana wa Mtu."  

 

 

--

John 2

 

 

 

 

HTMLBible Software - Public Domain Software by johnhurt.com

 


Other Items are Available At These Sites: