Swahili New Testament Bible

John 9

John

Return to Index

Chapter 10

1


 

  Yesu alisema "Kweli nawaambieni, yeyote yule asiyeingia katika zizi la kondoo kwa kupitia mlangoni, bali hupenya na kuingia kwa njia nyingine, huyo ni mwizi na mnyang`anyi.  

 

 

--

2


 

  Lakini anayeingia kwa kupitia mlangoni, huyo ndiye mchungaji wa kondoo.  

 

 

--

3


 

  Mngoja mlango wa zizi humfungulia, na kondoo husikia sauti yake, naye huwaita kondoo wake kila mmoja kwa jina lake na kuwaongoza nje.  

 

 

--

4


 

  Akisha watoa nje huwatangulia mbele nao kondoo humfuata, kwani wanaijua sauti yake.  

 

 

--

5


 

  Kondoo hao hawawezi kumfuata mgeni, bali watamkimbia kwa sababu hawaijui sauti yake."  

 

 

--

6


 

  Yesu aliwaambia mfano huo, lakini wao hawakuelewa alichotaka kuwaambia.  

 

 

--

7


 

  Basi, akasema tena, "Kweli nawaambieni, mimi ni mlango wa kondoo.  

 

 

--

8


 

  Wale wengine wote waliokuja kabla yangu ni wezi na wanyang`anyi, nao kondoo hawakuwasikiliza.  

 

 

--

9


 

  Mimi ni mlango. Anayeingia kwa kupitia kwangu ataokolewa; ataingia na kutoka, na kupata malisho.  

 

 

--

10


 

  Mwizi huja kwa shabaha ya kuiba, kuua na kuharibu. Mimi nimekuja mpate kuwa na uzima--uzima kamili.  

 

 

--

11


 

  "Mimi ni mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo wake.  

 

 

--

12


 

  Mtu wa kuajiriwa ambaye si mchungaji, na wala kondoo si mali yake, anapoona mbwa mwitu anakuja, huwaacha kondoo na kukimbia. Kisha mbwa mwitu huwakamata na kuwatawanya.  

 

 

--

13


 

  Yeye hajali kitu juu ya kondoo kwa sababu yeye ni mtu wa mshahara tu.  

 

 

--

14


 

  Mimi ni mchungaji mwema. Nawajua walio wangu, nao walio wangu wananijua mimi,  

 

 

--

15


 

  kama vile Baba anijuavyo, nami nimjuavyo Baba. Mimi nayatoa maisha yangu kwa ajili yao.  

 

 

--

16


 

  Tena ninao kondoo wengine ambao hawamo zizini humu. Inanibidi kuwaleta hao pia, nao wataisikia sauti yangu, na kutakuwako kundi moja na mchungaji mmoja.  

 

 

--

17


 

  "Baba ananipenda kwani nautoa uhai wangu ili nipate kuupokea tena.  

 

 

--

18


 

  Hakuna mtu anayeninyang`anya uhai wangu; mimi na nautoa kwa hiari yangu mwenyewe. Ninao uwezo wa kuutoa na uwezo wa kuuchukua tena. Hivi ndivyo Baba alivyoniamuru nifanye."  

 

 

--

19


 

  Kukawa tena na mafarakano kati ya Wayahudi kwa sababu ya maneno haya.  

 

 

--

20


 

  Wengi wao wakasema, "Ana pepo; tena ni mwendawazimu! Ya nini kumsikiliza?"  

 

 

--

21


 

  Wengine wakasema, "Haya si maneno ya mwenye pepo. Je, pepo anaweza kuyafumbua macho ya vipofu?"  

 

 

--

22


 

  Huko Yerusalemu kulikuwa na sikukuu ya Kutabaruku. Wakati huo ulikuwa wa baridi.  

 

 

--

23


 

  Naye Yesu akawa anatembea Hekaluni katika ukumbi wa Solomoni.  

 

 

--

24


 

  Basi, Wayahudi wakamzunguka, wakamwuliza, "Utatuacha katika mashaka mpaka lini? Kama wewe ndiye Kristo, basi, tuambie wazi."  

 

 

--

25


 

  Yesu akawajibu, "Nimewaambieni, lakini hamsadiki. Kazi ninazozifanya mimi kwa jina la Baba yangu zinanishuhudia.  

 

 

--

26


 

  Lakini ninyi hamsadiki kwa sababu ninyi si kondoo wangu.  

 

 

--

27


 

  Kondoo wangu huisikia sauti yangu; mimi nawajua, nao hunifuata.  

 

 

--

28


 

  Mimi nawapa uzima wa milele; nao hawatapotea milele, wala hakuna mtu atakayeweza kuwatoa mkononi mwangu.  

 

 

--

29


 

  Baba yangu ambaye ndiye aliyenipa hao ni mkuu kuliko wote, wale hakuna awezaye kuwatoa mikononi mwake Baba.  

 

 

--

30


 

  Mimi na Baba, tu mmoja."  

 

 

--

31


 

  Basi, Wayahudi wakachukua mawe ili wamtupie.  

 

 

--

32


 

  Yesu akawaambia, "Nimewaonyesheni kazi nyingi kutoka kwa Baba. Ni ipi kati ya hizo inayowafanya mnipige mawe?"  

 

 

--

33


 

  Wayahudi wakamjibu, "Hatukupigi mawe kwa ajili ya tendo jema, ila kwa sababu ya kukufuru! Maana wajifanya kuwa Mungu hali wewe ni binadamu tu."  

 

 

--

34


 

  Yesu akawajibu, "Je, haikuandikwa katika Sheria yenu: `Mimi nimesema, ninyi ni miungu?`  

 

 

--

35


 

  Mungu aliwaita miungu wale waliopewa neno lake; nasi twajua kwamba Maandiko Matakatifu yasema ukweli daima.  

 

 

--

36


 

  Je, yeye ambaye Baba alimweka wakfu na kumtuma ulimwenguni, mnamwambia: `Unakufuru`, eti kwa sababu nilisema: `Mimi ni Mwana wa Mungu?`  

 

 

--

37


 

  Kama sifanyi kazi za Baba yangu msiniamini.  

 

 

--

38


 

  Lakini ikiwa ninazifanya, hata kama hamniamini, walau ziaminini hizo kazi mpate kujua na kutambua kwamba Baba yuko ndani yangu, nami niko ndani yake."  

 

 

--

39


 

  Wakajaribu tena kumkamata lakini akachopoka mikononi mwao.  

 

 

--

40


 

  Yesu akaenda tena ng`ambo ya mto Yordani, mahali Yohane alipokuwa akibatiza, akakaa huko.  

 

 

--

41


 

  Watu wengi walimwendea wakasema, "Yohane hakufanya ishara yoyote. Lakini yale yote Yohane aliyosema juu ya mtu huyu ni kweli kabisa."  

 

 

--

42


 

  Watu wengi mahali hapo wakamwamini.  

 

 

--

John 11

 

 

 

 

HTMLBible Software - Public Domain Software by johnhurt.com

 


Other Items are Available At These Sites: