Swahili New Testament Bible

John 14

John

Return to Index

Chapter 15

1


 

  "Mimi ni mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima.  

 

 

--

2


 

  Yeye huliondoa ndani yangu kila tawi lisilozaa matunda, na kila tawi lizaalo hulisafisha lipate kuzaa zaidi.  

 

 

--

3


 

  Ninyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya ule ujumbe niliowaambieni.  

 

 

--

4


 

  Kaeni ndani yangu, nami nikae ndani yenu. Tawi haliwezi peke yake kuzaa matunda lisipokaa katika mzabibu hali kadhalika nanyi hamwezi kuzaa matunda msipokaa ndani yangu. ic  

 

 

--

5


 

  "Mimi ni mzabibu, nanyi ni matawi yake. Akaaye ndani yangu, nami ndani yake, huyo atazaa matunda mengi, maana bila mimi hamwezi kufanya chochote.  

 

 

--

6


 

  Mtu yeyote asipokaa ndani yangu hutupwa nje kama tawi litupwalo nje hata likakauka. Watu huliokota tawi la namna hiyo na kulitupa motoni liungue.  

 

 

--

7


 

  Mkikaa ndani yangu na maneno yangu yakikaa ndani yenu, basi, ombeni chochote mtakacho nanyi mtapewa.  

 

 

--

8


 

  Baba yangu hutukuzwa kama mkizaa matunda mengi na kuwa wanafunzi wangu.  

 

 

--

9


 

  Mimi nimewapenda ninyi kama vile Baba alivyonipenda mimi. Kaeni katika pendo langu.  

 

 

--

10


 

  Mkizishika amri zangu mtakaa katika pendo langu, kama vile nami nilivyozishika amri za Baba yangu na kukaa katika pendo lake.  

 

 

--

11


 

  Nimewaambieni mambo haya ili furaha yangu ikae ndani yenu, na furaha yenu ikamilike.  

 

 

--

12


 

  Hii ndiyo amri yangu: pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda ninyi.  

 

 

--

13


 

  Hakuna upendo mkuu zaidi kuliko upendo wa mtu atoaye uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.  

 

 

--

14


 

  Ninyi ni rafiki zangu mkifanya ninayowaamuru.  

 

 

--

15


 

  Ninyi siwaiti tena watumishi, maana mtumishi hajui anachofanya bwana wake. Lakini mimi nimewaita ninyi rafiki, kwa sababu nimewajulisha yote ambayo nimeyasikia kutoka kwa Baba yangu.  

 

 

--

16


 

  Ninyi hamkunichagua mimi; mimi niliwachagueni na kuwatuma mwende mkazae matunda, matunda yadumuyo, naye Baba apate kuwapa ninyi chochote mumwombacho kwa jina langu.  

 

 

--

17


 

  Basi, amri yangu kwenu ndiyo hii: pendaneni.  

 

 

--

18


 

  "Kama ulimwengu ukiwachukia ninyi, kumbukeni kwamba umenichukia mimi kabla haujawachukia ninyi.  

 

 

--

19


 

  Kama mngalikuwa watu wa ulimwengu, ulimwengu ungaliwapenda ninyi kama watu wake. Lakini kwa vile ninyi si wa ulimwengu, ila mimi nimewachagueni kutoka ulimwenguni, kwa sababu hiyo ulimwengu unawachukieni.  

 

 

--

20


 

  Kumbukeni niliyowaambieni: mtumishi si mkuu zaidi kuliko bwana wake. Ikiwa wamenitesa mimi, watawatesa na ninyi pia; kama wameshika neno langu, watalishika na lenu pia.  

 

 

--

21


 

  Lakini hayo yote watawatendeeni ninyi kwa sababu ya jina langu, kwani hawamjui yeye aliyenituma.  

 

 

--

22


 

  Kama nisingalikuja na kusema nao wasingalikuwa na hatia; lakini sasa hawawezi kujitetea kwamba hawana dhambi.  

 

 

--

23


 

  Anayenichukia mimi, anamchukia na Baba yangu pia.  

 

 

--

24


 

  Kama nisingalifanya kwao mambo ambayo hakuna mtu mwingine amekwisha yafanya wasingalikuwa na hatia; lakini sasa wameona niliyoyafanya wakinichukia mimi, wakamchukia na Baba yangu pia.  

 

 

--

25


 

  Na hivi ni lazima yatimie yale yaliyoandikwa katika Sheria yao: `Wamenichukia bure!`  

 

 

--

26


 

  "Atakapokuja huyo Msaidizi nitakayemtuma kwenu kutoka kwa Baba, huyo Roho wa kweli atokaye kwa Baba, yeye atanishuhudia mimi.  

 

 

--

27


 

  Nanyi pia mtanishuhudia kwa kuwa mmekuwa nami tangu mwanzo.  

 

 

--

John 16

 

 

 

 

HTMLBible Software - Public Domain Software by johnhurt.com

 


Other Items are Available At These Sites: