Swahili New Testament Bible

Romans 11

Romans

Return to Index

Chapter 12

1


 

  Kwa hiyo, ndugu zangu, maadam Mungu ni mwenye huruma nyingi, nawasihi kwa moyo wote: jitoleeni nafsi zenu kwa Mungu kama tambiko iliyo hai, takatifu na yenye kupendeza. Hii ndiyo njia yenu halisi ya kumwabudu.  

 

 

--

2


 

  Msiige mitindo ya ulimwengu huu, bali Mungu afanye mabadiliko ndani yenu kwa kuzigeuza fikira zenu. Hapo ndipo mtakapoweza kuyajua mapenzi ya Mungu, kutambua jambo lililo jema, linalompendeza na kamilifu.  

 

 

--

3


 

  Kutokana na neema aliyonijalia Mungu, nawaambieni ninyi nyote: msijione kuwa ni kitu zaidi kuliko mnavyopaswa kuwa. Fikira zenu na ziwe na kiasi kufuatana na kipimo cha imani Mungu aliyomgawia kila mmoja.  

 

 

--

4


 

  Mwili una viungo vingi, kila kimoja na kazi yake.  

 

 

--

5


 

  Hali kadhalika ingawa sisi ni wengi, tu mwili mmoja kwa kuungana na Kristo, na kila mmoja ni kiungo cha mwenzake.  

 

 

--

6


 

  Basi, tunavyo vipaji mbalimbali kufuatana na neema tuliyopewa. Mwenye kipaji cha unabii na akitumie kadiri ya imani yake.  

 

 

--

7


 

  Mwenye kipaji cha utumishi na atumikie. mwenye kipaji cha kufundisha na afundishe.  

 

 

--

8


 

  Mwenye kipaji cha kuwafariji wengine na afanye hivyo. Mwenye kumgawia mwenzake alicho nacho na afanye hivyo kwa ukarimu. Msimamizi na asimamie kwa bidii; naye mwenye kutenda jambo la huruma na afanye hivyo kwa furaha.  

 

 

--

9


 

  Mapendo yenu na yawe bila unafiki wowote. Chukieni jambo lolote ovu, zingatieni jema.  

 

 

--

10


 

  Pendaneni kidugu; kila mmoja amfikirie mwenzake kwanza kwa heshima.  

 

 

--

11


 

  Msilegee katika bidii, muwe wachangamfu rohoni katika kumtumikia Bwana.  

 

 

--

12


 

  Tumaini lenu liwaweke daima wenye furaha; muwe na saburi katika shida na kusali daima.  

 

 

--

13


 

  Wasaidieni watu wa Mungu katika mahitaji yao; wapokeeni wageni kwa ukarimu.  

 

 

--

14


 

  Watakieni baraka wote wanaowadhulumu ninyi; naam, watakieni baraka na wala msiwalaani.  

 

 

--

15


 

  Furahini pamoja na wanaofurahi, lieni pamoja na wanaolia.  

 

 

--

16


 

  Muwe na wema uleule kwa kila mtu. Msijitakie makuu, bali jishugulisheni na watu wadogo. Msijione kuwa wenye hekima sana.  

 

 

--

17


 

  Msilipe ovu kwa ovu. Zingatieni mambo mema mbele ya wote.  

 

 

--

18


 

  Kadiri inavyowezekana kwa upande wenu, muwe na amani na watu wote.  

 

 

--

19


 

  Wapenzi wangu, msilipize kisasi, bali mwachieni Mungu jambo hilo; maana Maandiko Matakatifu yasema: "Kulipiza kisasi ni shauri langu; mimi nitalipiza asema Bwana."  

 

 

--

20


 

  Tena, Maandiko yasema: "Adui yako akiwa na njaa, mpe chakula; akiwa na kiu, mpe kinywaji. Maana kwa kufanya hivyo utamfanya apate aibu kali kama makaa ya moto juu ya kichwa chake."  

 

 

--

21


 

  Usikubali kushindwa na ubaya, bali ushinde ubaya kwa wema.  

 

 

--

Romans 13

 

 

 

 

HTMLBible Software - Public Domain Software by johnhurt.com

 


Other Items are Available At These Sites: