Swahili New Testament Bible

1st Thessalonians 4

1 Thessalonians

Return to Index

Chapter 5

1


 

  Ndugu, hakuna haja ya kuwaandikieni juu ya nyakati na majira yatakapotukia mambo haya.  

 

 

--

2


 

  Maana ninyi wenyewe mwajua kwamba Siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajavyo usiku.  

 

 

--

3


 

  Watu watakapokuwa wanasema: "Kila kitu ni shwari na salama" ndipo uharibifu utakapowaangukia ghafla! Mambo hayo yatatukia ghafla kama uchungu wa uzazi unavyomjia mama anayejifungua, wala watu hawataweza kuepukana nayo.  

 

 

--

4


 

  Lakini ninyi ndugu, hamko gizani, na siku hiyo haipaswi kuwajieni ghafla kama vile mwizi.  

 

 

--

5


 

  Ninyi nyote ni watu mnaoishi katika mwanga, watu wa mchana. Sisi si watu wa usiku, wala wa giza.  

 

 

--

6


 

  Basi, tusilale usingizi kama wengine; tunapaswa kukesha na kuwa na kiasi.  

 

 

--

7


 

  Wanaolala hulala usiku, na walevi hulewa usiku.  

 

 

--

8


 

  Lakini sisi ni watu wa mchana na tunapaswa kuwa na kiasi. Tunapaswa kuvaa imani na upendo kama vazi la kujikinga kifuani, na tumaini letu la wokovu kama kofia ya chuma.  

 

 

--

9


 

  Maana Mungu hakututeua ili tuangamizwe na ghadhabu yake, bali tuupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,  

 

 

--

10


 

  ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, iwe tu hai au tumekufa.  

 

 

--

11


 

  Kwa hiyo farijianeni na kusaidiana ninyi kwa ninyi kama mnavyofanya sasa.  

 

 

--

12


 

  Ndugu, tunawaombeni muwastahi wale wanaofanya kazi kati yenu, wale wanaowaongoza na kuwafundisheni kuhusu maisha ya Kikristo.  

 

 

--

13


 

  Wapeni heshima kubwa na kuwapenda kwa sababu ya kazi wanayofanya. Muwe na amani kati yenu.  

 

 

--

14


 

  Ndugu, tunawahimizeni muwaonye watu walio wavivu, muwatie moyo watu wanyonge, muwasaidie watu dhaifu, muwe na subira kwa wote.  

 

 

--

15


 

  Angalieni mtu yeyote asimlipe mwingine maovu kwa maovu, ila nia yenu iwe kutendeana mema daima na kuwatendea mema watu wote.  

 

 

--

16


 

  Furahini daima,  

 

 

--

17


 

  salini kila wakati  

 

 

--

18


 

  na muwe na shukrani katika kila hali. Hayo ndiyo anayotaka Mungu kwenu katika kuungana kwenu na Kristo Yesu.  

 

 

--

19


 

  Msimpinge Roho Mtakatifu;  

 

 

--

20


 

  msidharau unabii.  

 

 

--

21


 

  Pimeni kila kitu: zingatieni kilicho chema,  

 

 

--

22


 

  na epukeni kila aina ya uovu.  

 

 

--

23


 

  Mungu anayetupatia amani awafanye ninyi watakatifu kwa kila namna na kuzilinda nafsi zenu--roho, mioyo na miili yenu--mbali na hatia yoyote wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.  

 

 

--

24


 

  Yeye anayewaita ninyi atafanya hivyo kwani ni mwaminifu.  

 

 

--

25


 

  Ndugu, tuombeeni na sisi pia.  

 

 

--

26


 

  Wasalimuni ndugu wote kwa ishara ya upendo.  

 

 

--

27


 

  Nawahimizeni kwa jina la Bwana muwasomee ndugu zetu wote barua hii.  

 

 

--

28


 

  Tunawatakieni neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.  

 

 

--

2nd Thessalonians 1

 

 

 

 

HTMLBible Software - Public Domain Software by johnhurt.com

 


Other Items are Available At These Sites: