Swahili New Testament Bible

James 1

James

Return to Index

Chapter 2

1


 

  Ndugu zangu, mkiwa mnamwamini Bwana Yesu Kristo, Bwana wa utukufu, msiwabague watu kamwe.  

 

 

--

2


 

  Tuseme mtu mmoja ambaye amevaa pete ya dhahabu na mavazi nadhifu anaingia katika mkutano wenu, na papo hapo akaingia mtu maskini aliyevaa mavazi machafu.  

 

 

--

3


 

  Ikiwa mtamstahi zaidi yule aliyevaa mavazi ya kuvutia na kumwambia: "Keti hapa mahali pazuri," na kumwambia yule maskini: "Wewe, simama huko," au "Keti hapa sakafuni miguuni pangu,"  

 

 

--

4


 

  je, huo si ubaguzi kati yenu? Je, na huo uamuzi wenu haujatokana na fikira mbaya?  

 

 

--

5


 

  Ndugu zangu wapenzi, sikilizeni! Mungu amechagua watu ambao ni maskini katika ulimwengu huu ili wapate kuwa matajiri katika imani na kupokea Utawala aliowaahidia wale wanaompenda.  

 

 

--

6


 

  Lakini ninyi mnawadharau watu maskini! Je, matajiri si ndio wanaowakandamizeni na kuwapeleka mahakamani?  

 

 

--

7


 

  Je, si haohao wanaolitukana hilo jina lenu zuri mlilopewa?  

 

 

--

8


 

  Kama mnaitimiza ile sheria ya Utawala kama ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: "Mpende binadamu mwenzako kama unavyojipenda wewe mwenyewe", mtakuwa mnafanya vema kabisa.  

 

 

--

9


 

  Lakini mkiwabagua watu, basi, mwatenda dhambi, nayo Sheria inawahukumu ninyi kuwa mna hatia.  

 

 

--

10


 

  Anayevunja amri mojawapo ya Sheria, atakuwa na hatia ya kuivunja Sheria yote.  

 

 

--

11


 

  Maana yuleyule aliyesema: "Usizini," alisema pia "Usiue". Kwa hiyo, hata ikiwa hukuzini lakini umeua, wewe umeivunja Sheria.  

 

 

--

12


 

  Basi, semeni na kutenda kama watu watakaohukumiwa kwa sheria iletayo uhuru.  

 

 

--

13


 

  Maana, Mungu hatakuwa na huruma atakapomhukumu mtu asiyekuwa na huruma. Lakini huruma hushinda hukumu.  

 

 

--

14


 

  Ndugu zangu, kuna faida gani mtu kusema ana imani, lakini haonyeshi kwa vitendo? Je, hiyo imani yawezaje kumwokoa?  

 

 

--

15


 

  Tuseme kaka au dada hana nguo au chakula.  

 

 

--

16


 

  Yafaa kitu gani ninyi kuwaambia hao: "Nendeni salama mkaote moto na kushiba," bila kuwapatia mahitaji yao ya maisha?  

 

 

--

17


 

  Vivyo hivyo, imani peke yake bila matendo imekufa.  

 

 

--

18


 

  Lakini mtu anaweza kusema: "Wewe unayo imani, mimi ninayo matendo!" Haya! Nionyeshe jinsi mtu anavyoweza kuwa na imani bila matendo, nami nitakuonyesha imani yangu kwa matendo yangu.  

 

 

--

19


 

  Je, wewe unaamini kwamba yuko Mungu mmoja? Sawa! Lakini hata pepo huamini hilo, na hutetemeka kwa hofu.  

 

 

--

20


 

  Mpumbavu wee! Je, wataka kuonyeshwa kwamba imani bila matendo imekufa?  

 

 

--

21


 

  Je, Abrahamu baba yetu alipataje kukubalika mbele yake Mungu? Kwa matendo yake, wakati alipomtoa mwanae Isaka sadaka juu ya madhabahu.  

 

 

--

22


 

  Waona basi, kwamba imani yake iliandamana na matendo yake; imani yake ilikamilishwa kwa matendo yake.  

 

 

--

23


 

  Hivyo yakatimia yale Maandiko Matakatifu yasemayo: "Abrahamu alimwamini Mungu na kwa imani yake akakubaliwa kuwa mtu mwadilifu; na hivyo Abrahamu akaitwa rafiki wa Mungu."  

 

 

--

24


 

  Mnaona basi, kwamba mtu hukubaliwa kuwa mwadilifu kwa matendo yake na si kwa imani peke yake.  

 

 

--

25


 

  Ilikuwa vivyo hivyo kuhusu yule malaya Rahabu; yeye alikubaliwa kuwa mwadilifu kwa sababu aliwapokea wale wapelelezi na kuwasaidia waende zao kwa kupitia njia nyingine.  

 

 

--

26


 

  Basi, kama vile mwili bila roho umekufa, vivyo hivyo imani bila matendo imekufa.  

 

 

--

James 3

 

 

 

 

HTMLBible Software - Public Domain Software by johnhurt.com

 


Other Items are Available At These Sites: